Posts

Showing posts from December, 2013

Klabu bingwa

Image
Klabu bingwa ya ni Raja au Bayern? Timu ya Raja Casablanca kutoka Morocco imefuzu kucheza fainali za klabu bingwa ya dunia baada ya kuisambaratisha Atletico Mineiro kutoka Brazil katika mchezo wa nusu fainali. Raja waliweza kufunga magoli mawili katika dakika 10 za mwisho katika mchezo huo. Taarifa zinazohusiana FIFA ,  Kandanda Kwa matokeo hayo Raja Casablanca watamenyana na Bayern Munich ya Ujerumani katika mchezo wa fainali. Raja ndio waliokuwa wa kwanza kujipatia bao lililofungwa na Mouhssine Lajour. Mchezaji wa zamani wa Barcelona Ronaldinho alipiga kiufundi mpira wa adhabu na kuisawazishia bao timu yake ya Mineiro. Lakini Mohaine Moutaouali aliiweka mbele timu yake ya Raja baada ya kufunga mpira wa penalti, huku Vivien Mabide akikamilisha ushindi wa magoli 3 ya Raja dhidi ya 1 la Mineiro. Kivutio katika mchezo ni kwa wachezaji wa Raja kumzunguka Ronaldinho mara baada ya kupigwa filimbi ya kumaliza mchezo, huku wakimbusu na jezi na viatu vyake kam...

Uganda:Mashoga,wasagaji kufungwa maisha

Image
Uganda:Mashoga,wasagaji kufungwa maisha Iwapo Rais Yoweri Museveni ataidhinisha sheria hiyo inamaanisha atakayepatkana na hatia atahukumiwa kifungo cha maisha gerezani. Wakati hu huo bunge hilo hilo la Uganda siku ya Alhamisi liliidhinisha mswaada unaopiga marufuku maonyesho ya picha za chafu.Mswaada huo uliopitishwa na bunge siku ya Ijumaa halikadhalika inasema mtu yeyote aliye na taarifa za watu wanoshiriki mapenzi ya jinsia moja na kushindwa kuripoti habari hizo kwa maafisa wa polisi atafungwa gerezeni maisha. Mswada huo unaharamisha kitu chochote kitakachoonyesha sehemu nyeti kama vile matiti, mapaja, makalio au tabia yoyote inayozua uchu wa mapenzi. Kulingana na mswada huo, sheria iliyopo sasa kuhusu picha chafu haihusu zaidi picha hizo bali linahusu uchapishaji ,mawasiliano, taarifa , burudani, maonyesho katika kumbi za kuigizia, miziki inyochezwa katika vyombo vya habari, densi, sanaa, mitindo na picha za runinga. Mapema mwaka huu Waziri wa maadili wa Uganda, Simon ...