Posts

Showing posts from January, 2013

Ghana yapiga marufuku majokofu mitumba

Image
Serikali ya Ghana imepiga marufuku uagizaji wa majokofu yaliyotumika au mitumba ili kupunguza matumizi ya nishati na uchafuzi wa mazingira. Wafanyabiashara wa majokofu Ghana Majokofu mengi kukuu yana kemikali inayoitwa Chlorofluorocarbons (CFCs) inayoharibu mazingira. Licha ya kuwa bidhaa hizo zimepigwa marufuku, na hazitengenezwi tena, majokofu hayo yanaaminika kutumika barani Afrika. Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Nishati ya Ghana ameimbia BBC kuwa marufuku hiyo, imelifanya taifa lao kuwa kielelezo katika kanda ya Afrika Magharibi. Sheria ya kupiga marufuku majokofu hayo iliidhinishwa mwaka wa 2008, lakini muda wake uliongezwa ili kuwa na wauzaji wa bidhaa hizo kufanya marekebisho. Hata hivyo wafanyabiashara kadha nchini Ghana wameshutumu uamuzi huo wa serikali wakisema idadi kubwa ya watu watak...

Kifaa cha Tablet kutoka Afrika

Image
Kifaa cha Tablet kilichoundwa barani Afrika Simu aina ya smartphone na kompyuta za tablet zinazosemekana kuwa vifaa vya mawasiliano vya kwanza kutengenezwa na kampuni ya Afrika zimezinduliwa. Vifaa hivyo, ambavyo vimebuniwa na mjasiriamali wa Congo,vinatengenezwa nchini China. Kampuni yake ya VMK, vifaa vyake vinaendeshwa kwa teknolojia ya Android ya Googles. Simu hizo za smartphone zitauzwa kwa bei ya rejareja ya dola $170, sawa na pauni za Uingereza (£105) na kompyuta itauzwa kwa dola $300 sawa na pauni (£185). "Ni Waafrika wenyewe, ndiyo watakaofahamu mahitaji ya Afrika," amesema Bwana Mankou katika mkutano wa Tech4Africa mjini Johannesburg. "Apple ni kampuni kubwa Marekani, Samsung ni barani Asia na tunataka VMK kuwa kampuni kubwa barani Afrika." Kifaa cha Tablet kilichoundwa barani Afrika Blogu ya teknolojia ya Smartplanet imeripoti kuwa kompyuta za VMK zinatoa huduma ya uunganishaji wa wi-fi na uwezo wa gig...

Toure mchezaji bora Afrika mwaka huu

Image
Yahya Toure Mcheza kiungo wa Manchester City Yaya Toure ametangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya mchezaji bora barani Afrika kwa mwaka wa pili mfululizo. Toure alimshinda noadha wa Ivory Coast na mshambulizi wa zamani wa Chelsea Didier Drogba na aliyekuwa mlinda lango wa Arsenal Alex Song. Drogba alimaliza katika nafasi ya pili naye Song akawa wa tatu, katika uteuzi uliofanywa na makocha na maafisa wa kiufundi wa timu za soka barani Afrika ambazo ni wanachama wa shirikisho la mchezo wa soka barani Afrika CAF. Aliyekuwa mshambulizi wa Barcelona Samuel Eto'o ndiye anayeshikilia rekodi ya kushinda tuzo hiyo mara nyingi. Didier Drogba Eto'o ameshinda tuzo hiyo mara nne. Mabingwa wa soka barani Afrika, Zambia walituzwa kuwa timu bora barani mwaka huu na kocha wao Herve Renard naye aliteu...

Kesi dhidi ya Cecil yafutiliwa mbali Uganda

Image
David Cecil akiwa korokoroni Mahakama moja nchini Uganda, imefutilia mbali kesi dhidi ya mwandishi mmoja wa michezo ya tamthilia, David Cecil, ambaye alikuwa akikabiliwa na shtaka la kuonyesha mchezo kuhusu hali ya wapenzi wa jinsia moja, katika mji mkuu wa nchi hiyo Kampala. Bwana Cecil, alikabiliwa na tuhuma za kukiuka sheria kwa makusudi. Bwana Cecil ameiambia BBC, kuwa kesi hiyo ilifutiliwa mbali kutokana na kile alichokitaja kama ukosefu wa ushahidi wa kutosha dhidi yake. Mshukiwa huyo alikamatwa mwezi Septemba, kwa kukiuka sheria za hiyo kwa kuonyesha mchezo huo bila kibali wenye maudhui ''The River and the Mountain'' Mapenzi ya jinsia moja imeharamishwa nchini Uganda. Bunge la nchi hiyo linajadili uwezekano kwa kuimarisha adhabu ya wale watakaopatikana wakijihusisha na mapenzi ya jinsia moja. ...

Wanajeshi wa kigeni watumwa Afrika ya Kati

Image
Wanajeshi wa waasi katika Jamuhuri ya Afrika ya Kati Jeshi la eneo la Afrika FOMAC katika Jamhuri ya ya Afrika ya kati kwa sasa linaimarishwa na vikosi vya mataifa jirani wakijumuisha wanajeshi elfu mia moja na ishirini kutoka Jamuhuri ya Demokrasi ya Congo DRC. Kamanda wa FOMAC, amesema kuwa wanjeshi hao wataenda kuulinda mji wa Damara, dhidi ya waasi wanokaribia jiji kuu la Bangii. Ripoti zinasema wanajeshi hao wa waasi wafika takriban kilomita sabini na tano hivi kutoka mji mkuu wa Bangui. Msemaji wa waasi hao jijini Paris, anasema ameliambia shirika la Reuters kuwa wamesitisha kidogo safari yao na huenda wakajianda kwa mazungumzo ili kupata suluhu ya kisiasa. Serikali ya Gabon imesema kuwa itatuma kikosi cha wanajeshi 120, huku serikali ya Cameroon vile vile ikitarajiwa kutuma kiasi kama hicho Hili ndilo tishio k...

BREAKING NEWS

Image
Naamini chenye mwanzo siku zote hakikosi mwisho,hivyo basi sisi sote tutaelekea mahali anapopenda mweanyezimungu, na pia unatakiwa utambue ya kwamba pesa hutafutwa lakini binadamu kamwe hawezi kutafutwa,kama ilikuwa 50,000,000 hikuweza kumsaidia chochote,ingawa watu wanasema kutoa ni moyo walal si utajiri,innlilah wainlilah ljuni,mungu ametoa na mungu ametwaa jina la mungu liimiliwe AMEN!!!!!!!!!!!!!!!!!!!