Posts

Showing posts from December, 2012

Mzozo kuhusu tuzo ya CECAFA

Image
Mchezaji wa Uganda akikabiliana na mchezaji wa Kenya Mshambulizi wa timu ta taifa ya soka ya Uganda Cranes, Uganda, Robert Ssentongo, ameteuliwa kuwa mchezaji bora wa mashindano ya CECAFA Tusker Senior Challenge Cup, yaliyomalizika mjini Kampala. Sentongo hata hivyo alifunga magoli manne pekee wakati wa mashindano hayo. Wachezaji waliofunga idadi magoli mengi kuliko Sentongo,Mrisho Ngassa na John Bocco wa timu ya Tanzania bara, walinyimwa tuzo hilo, na kamati ya ufundi ya mashindano hayo. Katika mashindano yaliyopita, mchezaji aliyefunga idadi kubwa ya magoli ndiye huibuka mshindi wa taji hilo, lakini mwaka huu mambo nchini Uganda yalikuwa tofauti. ''Ngassa na Bocco walifunga magoli matano kila mmoja na ilitarajiwa wangepewa tuzo ya mfungaji bora lakini katika hali ya kushangaza kamati ya CECAFA, ilimpa tuzo hilo mshambuliaji wa Uganda, Robert Ssentongo aliyefunga magoli manne'' Alisema kocha wa Kilimanjaro Stars. Katibu mkuu wa CECAFA akiwa na kome ...

Mikel aongezewa miaka mitano

Image
Kiungo cha kati wa Chelsea, John Obi Mikel, ametia saini mkataba mpya wa miaka mitando kuendelea kusakata gozi Stamford Bridge, hadi mwaka 2017. Mikel kuendelea kucheza Stamford Bridge kwa muda wa miaka mitano Klabu hicho cha ligi kuu ya Premier kilitangaza habari hizo siku ya Jumatano. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Nigeria alijiunga na Chelsea akiwa kijana mwenye umri wa miaka 19 mwaka 2006. Hadi wakati huu ameichezea Chelsea jumla ya mechi 261, na kushuhudia ushindi mara nyingi; ubingwa wa klabu bingwa barani Ulaya, medali nne za Kombe la FA, ushindi mmoja wa ligi kuu ya Premier, na Kombe la Ligi. "Nimepata ushindi nikiwa na Chelsea karibu katika mashindano yote makubwa, na miaka niliyoichezea Chelsea ni maalum sana kwangu, nikitwaa ushindi na wachezaji nyota kama Didier Drogba, John Terry na Frank Lampard ambao wameichezea Chelsea kwa muda mrefu," Mikel alielezea katika taarifa katika tovuti ya klabu (www.chelseafc.com). "Ushindi wa klabu bingw...

Nemanja Vidic hoi kwa jeraha

Image
Nahodha wa Manchester United Nemanja Vidic ana jeraha la goti Nahodha wa Manchester United Nemanja Vidic hatarejea uwanjani, kufuatia jeraha katika mechi ya ligi ya klabu bingwa barani Ulaya dhidi ya Cluj. Vidic, 31, hajacheza tangu kufanyiwa upasuaji wa goti mwezi Septemba lakini alikuwa ameratibiwa kucheza leo dhidi ya Waromania hao. Lakini sasa mlinzi huyo hatashiriki mechi hiyo na pia hatakuwepo Jumapili katika "Manchester Derby." Wayne Rooney ataanza katika kikosi tofauti sana, baada ya United kufuzu kama viongozi wa kundi H. Mkufunzi wa Manchester United Alex Ferguson alisema: " Sidhani Vidic atacheza. Anahisi anahitaji siku zingine kadhaa za mazoezi. "Hatacheza katika derby iwapo hatacheza kesho, licha ya kuwa sikutarajia kumshirikisha Jumapili. " Tutawapumzisha baadhi ya wachezaji lakini lazima tutende haki kwa timu zote zinazotarajia kufuzu kwa michuano tofauti- iwe ni katika ligi ya klabu bingwa barani Ulaya au Kombe la Uropa. ...

Messi avunja rekodi

Image
Chapisha Lionel Messi akisherehekea bao lake Mshambulizi matata wa Barcelona Lionel Messi, ameweka rekodi mpya kwa kufunga bao lake la 86 mwaka huu. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, kutoka Argentina, alivunja rekodi iliyowekwa na Gerd Mueller ya kufunga magoli 85 mwaka wa 1972 na kuweka rekodi mpya, ambayo pia inajumuisha idadi ya magoli aliyoyafungwa na timu yake ya taifa na klabu ya Barcelona. Messi alivunja rekodi hiyo baada ya kufunga magoli mawili wakati wa mechi yao dhidi ya Real Betis siku ya Jumapili, ambayo Barcelona ishinda kwa magoli mawili kwa moja. Baada ya dakika kumi na sita za mechi hiyo Messi alifunga bao la kwanza na kusawazisha rekodi hiyo, kabla ya kuongeza la pili kunako dakika ya 25 na kuweka rekodi mpya. Messi abebwa kwa machela Lionel Messi wakati alipojeruhiwa Juhudi za mchezaji huyo za kuvunja rekodi hiyo iliyowekwa na Mjerumani Mueller, zilionekana kuambulia patupu, baada ya mchezaji huyo kujeruhiwa na kubebwa kwa mach...

Je mashabiki wataruhusiwa kusimama?

Image
Mashabiki wa Soka wa Uingereza Kundi moja la mashabiki wa soka nchini Uingereza limesema kuwa vilabu kumi na vitatu nchini Uingereza vimesemekana kuunga mkono, uamuzi wa kuruhusu mashabiki kutizama mechi wakiwa wamesimama. Siku ya Jumanne, kundi hilo lilitarajia lipata uungwaji mkono kutoka kwa wabunge, kuhusu mipango yake ya kuifanyia pendekezo hilo majaribio wakati wa mechi za ligi kuu ya premier. Kundi hilo linaamini kuwa mpango uliopigwa marufuku baada ya mkasa uliotokea katika uwanja wa Hillsborough mwaka wa 1989, sasa ni salama. Awali wasimamizi wa ligi kuu ya Premier walisema kuwa hawataunga mkono pendekezo hilo. Msemaji wa kundi hilo la FSF, Peter Daykin asema'' Tunahitaji kuchunguza ikiwa itafaulu na njia ya pekee ya kupata jibu ni kwa kuijaribu'' Mkasa wa Hillsborough Tangu mwaka wa 1994, mamshabiki wote wa soka ni sharti waketi wakati mechi inapoendelea. Eneo la kumbukumbu ya mkasa wa Hillsborough Hii ni baada ya ripoti ya ka...

Chelsea yashindwa na Corinthians 1-0

Image
Twitter Tuma kwa rafiki yako Chapisha akisherehekea bao lake dhidi ya Chelsea Klabu ya Corrinthians kutoka Brazil, imeshinda kombe la klabu bingwa duniani baada ya kuilaza Chelsea bao moja kwa bila katika mechi ya fainali iliyochezwa nchini Japan. Paolo Guerrero aliifungia Corinthians, bao hilo muhimu na la ushindi. Hata hivyo Chelsea, ilipoteza bafasi nyingi za kufunga wakati wa mechi hiyo. Katika muda wa ziada Fernando Torres, alipoteza nafasi nzuri sana ya kuzawazisa licha ya kuwapiku walinzi wa Corinthians na kubakia kipa pekee. Torres alijaribu kumchenga kipa wa Corinthians lakini kombora lake likawa hafifu na kudakwa kwa urahisi na kipa. Chelsea ilimaliza mechi hiyo ikiwa na wachezaji kumi baada ya Gary Cahil, kupewa kadi nyekundu baada ya kumfanyika madhambi mchezaji wa Corrinthians Emerson. Bao la chelsea lililofuingwa kwa kichwa na Fernando torres lilikataliwa na hivyo vijana hao kutoka brazil wakaibuka na ushindi.

Park ashinda uchaguzi Korea Kusini

Image
Rais mteule wa Korea Kusini Park Geun-hye Rais mteule wa Korea Kusini , Park Geun-hye, amesema ushindi wake katika uchaguzi mkuu utasaidia uchumi wa taifa hilo kuimarika. Bi. Park, ambaye ni mwanawe, kiongozi wa kiimla wa zamani wa taifa hilo Parl Chung-hee, alimshinda mpinzani wake wa chama cha Liberal Moon Jae-in na kuwa kiongozi wa kwanza wa taifa hilo mwanamke. Kura bado zinaendelea kuhesabiwa, lakini Bwana Moon amekiri kushindwa. Idadi kubwa ya watu walijitokeza kupiga kura katika uchaguzi huo ambao masauala ya kiuchumi na kijamii yaliangaziwa pakubwa. Bi. Park, mwenye umri wa miaka 60, atamrithi Lee Myung-bak, ambaye anastaafu baada ya kukamilisha miaka mitano kama rais wa nchi hiyo kuambatana na sheria za nchi hiyo. Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na vyombo vya habari nchini h...

Kocha amtaka Adebayor kubadili uamuzi

Image
Emmanuel Adebayor akizungumza na refa Kocha wa Togo Didier Six amesema atafanya kila juhudi ili kumshawishi mshambulizi wa Tottenham, Emmanuel Adebayor kuichezea timu ya taifa ya Togo wakati wa michuano ya kombe la Mataifa bingwa Barani Afrika, mwezi ujao. Mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 28, alitangaza kustaafu kutoka kwa kechi zote za kimataifa, kwa sababu ya mzozo wake na shirikisho la mchezo wa soka, kuhusiana na malipo ya ziada. Six alisema'' nafanya kila juhudi ili niweze kumshawishi abadili uamuzi wake'' ''Yeye ni mchezaji wa hadhi ya juu na pia naodha wa timu yetu ya taifa. Adebayor ana jukumu kubwa kwa kikosi chetu'' aliongeza kocha huyp huyo. Msemaji wa mchezaji huyo, Amedodji Blaise mapema mwezi huu alisema Adebayor hatashiriki katika mechi yoyote ya kimataifa kwa muda usiojulikana na hata...

Raia wa Sudan akatwa kichwa Saudi Arabia

Image
Mji wa Mecca nchini Saudi Arabia Wizara ya mambo ya ndani nchini Saudi Arabia, imesema kuwa raia mmoja wa Sudan amenyongwa kwa kukatwa kichwa. Kwa mujibu wa tangazo kutoka kwa wizara hiyo, iliyochapishwa na shirika la habari la serikali, Othman Mohammed alinyongwa katika mji wa Magharibi wa Mecca. Mohammed alipatikana na hatia ya kumuua raia mwingine kutoka Sudan, Salah Ahmed kwa kumpiga vibaya kichwani. Chini ya sheria kali katika Ufalme huo wa Kiarabu, adhabu ya kifo hutolewa kwa makosa kadhaa, yakiwemo mauaji, ubakaji na ulanguzi wa madawa ya kulevya. Shirika la kutetea haki za kibinadam la Amnesty International limesema kuwa watu 89 walinyongwa nchini Saudi Arabia mwaka uliopita pekee.

Kagame aonywa dhidi ya kuwasaidia waasi

Image
Rais Barrack Obama wa Marekani ametoa wito kwa rais wa Rwanda Paul Kagame, kusitisha msaada anaotoa kwa makundi ya waasi nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Kwa mujibu wa ikulu ya White House, rais Obama alifanya mazungumzo ya simu ya Rais Paul Kagame siku ya jumanne, ambapo aliafiki tangazo lake la kujitolea katika harakati za kupatikana kwa amani katika Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo. Waasi wa M-23 wapo katika eneo la mashariki mwa Congo licha ya kuwepo kwa wanajeshi wa kutunza amani wa umoja wa mataifa katika eneo hilo. Ripoti ya hivi majuzi iliyochapishwa na Umoja wa Mataifa iliishutumu serikali ya Rwanda kwa kutoa msaada kwa waasi hao wa Congo, madai ambayo serikali ya Rwanda Imekanusha vikali. ...

Demba Ba kuhama Newcastle

Image
Mchezaji wa Newcastle Demba Ba Alan Pardew yuko tayari kumsajili mshambulizi wa Ukraine Artem Milevskiy ikiwa nyota wake Demba Ba hatasaini mkataba mpya na klabu hiyo. Kocha huyo wa Newcastle ameshindwa kumshawishi Demba Ba kusaini mkataba mpya na klabu hiyo. Klabu hiyo sasa inashauku nyingi kuhusiana na kipengee katika mkataba wake unaosema klabu yoyote inayotaka kumsajili mchezaji huyo kabla ya muda wake kumalizika ni sharti ili pauni milioni saba ikiwa atakihama klabu hiyo mwezi Januari mwakani. Pardew anafahamu wazi kuwa haitagharimu klabu yake hela nyingin kumsajili Milevskiy, 27, kutoka kwa klabu ya Dynamo Kiev. Klabu hiyo iliitisha pauni milioni 14 wakati Roy Hodgson alipojaribu kumsajili mchezaji huyo akiwa na klabu ya liverpool.

PREMIER LEAGUE TABLE

Image
  Team P W D L GD PTS 1 = Man Utd 17 14 0 3 19 42 2 = Man City 17 10 6 1 18 36 3 = Chelsea 16 8 5 3 11 29 4 = Tottenham 17 9 2 6 5 29 5 = Arsenal 17 7 6 4 13 27 6 = Everton 17 6 9 2 7 27 7 = West Brom 17 8 3 6 3 27 8 = Norwich 17 6 7 4 -6 25 9 = Stoke 17 5 9 3 2 24 10 = Swansea 17 6 5 6 4 23 11 = West Ham 17 6 5 6 1 23 12 = Liverpool 17 5 7 5 0 22 13 = Fulham 17 5 5 7 -1 20 14 = Aston Villa 17 4 6 7 -9 18 15 = Newcastle 17 4 5 8 -7 17 16 = Sunderland 17 3 7 7 -6 16 17 = Southampton 16 4 3 9 -10 15 18 = Wigan 17 4 3 10 -14 15 19 = QPR 17 1 7 9 -15 10 20 = Reading 17 1 6 10 -15 9  

ALAN PARDEW is ready to replace wantaway Demba Ba with Ukraine striker Artem Milevskiy.

Pards is a big Art fan Newcastle boss Pards has so far failed to talk Ba into signing a long-term deal. And Toon fear a £7million bid in January, triggering a buy-out clause in the Senegal star’s contract. But Pards knows Milevskiy, 27, can leave Dynamo Kiev on the cheap. Kiev wanted £14m when Roy Hodgson tried to sign him at Liverpool. Now his contract is running down and Kiev will take £6m rather than lose him for nothing in the summer. The striker’s agent Barry O’Connor confirmed: “There is plenty of interest from more than one club in England.” Read more: http://www.thesun.co.uk/sol/homepage/sport/football/4693359/Artem-Milevskiy-in-at-Newcastle-Demba-Ba-out.html#ixzz2FXfYslEu

Manchester United inamtaka Walcott

Image
Theo walcott Manchester United imesemekana kuwa inamsaka mcheza kiungo wa Arsenal Theo Walcott, mwenye umri wa miaka Ishirini na mitatu. Ripoti zinasema kuwa Manchester United inataka kumsajili Walcott sawa na walivyofanya na mshambulizi wa Arsenal Robin Van Persie mwezi Januari mwaka huu. Kocha wa Man United Sir Alex Ferguson ameripotiwa kuonyesha nia kubwa ya kumsajili mchezaji huyo ambaye mkataba wake na Arsenal unamazilika mswisho wa msimu huu.

EXCLUSIVE: Fergie set to beat City and Liverpool to Walcott as United lead race for Arsenal's contract rebel

Image
Manchester United have joined the race for Arsenal rebel Theo Walcott in a move similar to Robin van Persie's controversial switch to Old Trafford in August. Sir Alex Ferguson is keen to land the England winger, whose deal expires at the end of the season. Sportsmail understands that should Walcott leave Arsenal, his first choice would be United. Wanted man: Manchester United are leading the race to sign Theo Walcott   Walcott is declining to sign a five-year deal worth £75,000 a week, while formal talks over fresh terms have not taken place since August 28. He is said to be keen to stay but wants a deal closer to £100,000 a week. Liverpool, Manchester City and Chelsea are all interested, but United's keenness, along with Walcott's desire to join the Barclays Premier League leaders looks, looks to have put United in the driving seat. At the same time, Arsenal manager Arsene Wenger is exploring a January swoop for United misfit Nani, raising ...

Wafanyakazi wa afya wawili zaidi wauawa

Image
Raia wa Pakistanwakiomboleza kifo cha wafanyakazi wa afya Polisi nchini Pakistan wamesema kuwa watu waliojihami kwa bunduki wamewauwa watu wawili wanaohusika katika kampeni ya utoaji chanjo dhidi ya ugonjwa wa kupooza au polio, siku moja tu baada ya wafanyikazi watano wa afya kuuwawa kwa kupigwa risasi. Msemaji wa shirika la umoja wa mataifa kuhusu watoto UNICEF, amesema kuwa sasa wamelazimika kuahirisha kampeni hiyo kote nchini Pakistan, kutokana na sababu za kiusalama. Mashambulizi ya hivi punde katika mji wa Peshawar, yamepelekea mauaji ya mwanamke aliyekuwa akisimamia zoezi hilo la utoaji chanjo, dereva wake na mtu aliyekuwa akitoa chanjo. Viongozi wa Taliban wanasema kampeni hiyo dhidi ya ugonjwa wa polio ni kisingizio cha kufanya ujasuisi dhidi yao. Serikali ya Pakistan imesema haitakata tamaa katika juhudi za kutokomeza ugonjwa hu...

Kilimanjaro Stars kuvaana na Zambia

Image
Wachezaji wa timu ya Taifa ya Tanzania Siku chache tu, baada kumaliza katika nafasi ya nne kwenye mashindano ya CECAFA Senior Challenge Cup, Nchini Uganda, Timu taifa ya Tanzania iantarajiwa kurejea kambini kwa maandalizi ya mechi yao ya kirafiki dhidi ya mabingwa wa Afrika Zambia. Kwa mujibu wa shirikisho la mchezo wa soka nchini Tanzania, Kilimanjaro Stars itavaana na Chipolopolo tarehe 22 mwezi huu katika uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam. Kocha mkuu, Kim Poulsen tyari ametaja kikosi cha wachezaji 24 kitakachopiga kambi kujiandaa kwa mechi hiyo. Aidha kwa mara ya kwanza kikosi hicho kinajumishwa wachezaji waliotia for a kwenye michuanp ya ligi kuu na pia michuana ya CECAFA. Miongoni mwa wachezaji walioitwa kwa mara ya kwanza ni pamoja na Aishi Manul, Samih Nuhu, Issa Rashid na Mcha Khamis. Sita kati yao ni miongoni mwa wachezaji walioakilisha Zanzibar katika michuano ya CECAFA iliyomalizika siku ya Jumamosi jijini Kampala, Uganda, ambapo Zanzibar ilimaliza ...

England yailemea India

Image
Wachezaji wa Kriketi wa England England imekamilisha ushindi wake wa kwanza katika mashindano ya Kriketi kwa zaidi ya miaka 27 nchini India, huku wachezaji wawili wa Uingereza Jonathan Trott na Ian Bell wakiandikisha zaidi ya mikimbio mia mmoja kila mmoja katika mechi hiyo iliyochezwa mjini Nagpur. Trott aliweka mikimbio 143 naye Bell alipata 116 na kusalia hadi mwisho wa pambano hilo nna kuruhusu wenyeji wao India ambao walishindwa mjini Ahmedabad na kushinda mechi za Mumbaina Kolkata kupata sare iliyohitajika kuhakikisha ushindi wa England. India ilifanikiwa kumuondoa mchezaji mmoja tu wa England siku nzima na kutoa nafasi kwa Joe Root kucheza mechi yake ya kwanza na kuweka mikimbio 20. Awali England ilimaliza ikiwa na mikimbo 356 zaidi baada ya mchuano huo kumalizika huku wakiwa na mikimbio 352 baada ya kuwapoteza wachezaji wanne. Wachezaji wa England wanasema ushindi huo ulikuwa muhimu sana kwa kuwa walishindwa kwa wiketi tisa katika mechi yao ya kwanza lakin...

Kocha wa Simba afutwa kazi

Image
Aliyekuwa kocha wa Simba Wachezaji wa Simba wamepinga vikali uamuzi wa kamati kuu ya klabu wa kumfuta kazi kocha wa timu hiyo, Mserbia Milovan Cirkovic. wachezaji hao wanasema Cirkovic alikuwa na uwezo na ujuzi mkubwa na pia alikuwa na ushirikiano mwema na wachezaji. '' Kwa hakika sisi kama wachezaji tumeshangazwa sana na uamuzi wa viongozi wetu kwa kumsimamisha kazi kocha wetu ambaye tulikuwa na uhusiano mwema naye. Lakini kwa kuwa ni uamuzi ambao sisi hatuna mamlaka juu yake itabidi kuliheshimu ila kwa manung'uniko'' alisema mmoja wa wachezaji hao ambaye hakutaka kutajwa jina. Wachezaji wa Simba Wachezaji qa Simba wamehoji uamuzi huo wakisema ni nadra sana kuona kocha akifutwa kazi ili hali klabu inaandikisha matokeo mena. Lakini afisa mmoja wa klabu hiyo amesema kocha huyo amefutwa kazi kwa kuwa Simba kwa sasa haina uwezo wa kuendelea kumlipa mashahara wa kocha. Aliongeza kuwa Kocha Cirkovic alifutwa kazi kutokana na mtindo wake wa kut...

Balotelli kupinga uamuzi wa Man City

Image
Mario Balotelli akipewa kadi nyekundu wakati wa mechi yao na Arsenal Mshambulizi wa Manchester City Kutoka Italia, Mario Balotellu, atafika mbele ya kamati maalum ya shirikisho la mchezo wa soka nchini England siku ya Jumatano. Balotelli anapinga uamuzi wa klabu yake ya Manchester City ya kumpiga faini ya mshahara wake wa wiki mbili kuhusiana na rekodi yake mbovu ya nidhamu. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22, alikosa mechi 11 za ligi kuu na michuano ya ulaya msimu uliopita. Balotelli alikata rufaa kuhusu aumuzi huo, lakini kamati huru ya wanachama wa bodi ya wakurugenzi wa klabu hiyo wakaifutilia mbali. Balotteli anatarajiwa kufika mbele ya kikao hicho binfasi, pamoja na wakili wake kutoka Italia na mwakilishi mmoja wa chama cha wachezaji wa kulipwa, huku klabu ya manchester City ikialishwa na mawakili wake. Je Balotelli anastahili faini hiyo? David Bernstein mwenyekiti wa FA Faini hiyo ndicho kiwango cha juu zaidi kuambatana na kandarasi ya wachezaji,...

Kocha wa Harambee Stars ajiuzulu

Image
Aliyekuwa kocha wa Kenya Kocha wa Harambee Stars Henri Michel amejiuzulu miezi minne tu baada ya kusaini mkataba na shirikisho la mchezo wa soka nchini Kenya FKF. Kocha huyo kutoka Ufaransa, amekuwa kwenye mgomo baridi baada ya FKF kutomlipa mshahara wake wote. Michel hulipwa shillingi milioni nne na manaibu wake wawili nao hupokea mshahara wa milioni moja unusu. Kwa mujibu wa barua kutoka kwa Ubalozi wa Ufaransa mjini Nairobi kocha huyo anarejea nyumbani hii leo. Hata hivyo barua hiyo inaashirikia kuwa kocha huyo alijiuzulu tarehe kumi mwezi huu lakini tangazo hilo limetolewa leo tarehe 17 Desemba. Michel alikataa kuongoza Harambee Stars wakati wa michuano ya kuwania kombe la mataifa bingwa kanda ya Afrika Mashariki na Kati CECAFA, akiitaja mashindano hayo kama mashindano yasiyokuwa na maana yoyote. Aliyekuwa kocha wa Kenya Henri Mitchel Kocha huyo alisema jukumu lake kuu ni kuhakikisha Kenya imejianda vyema kwa michuano ya kuwania ubingwa wa mataifa ya Afr...

Mashabiki wakataa wachezaji weusi-Urussi

Image
Wachezaji wa Zenit ya Urussi Mashabiki wa klabu ya Zenit St Petersburg inayoshiriki katika ligi kuu ya premier nchini Urussi, wametoa wito kwa wasimamizi wa klabu hiyo kutowasajili wachezaji weusi na wale wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja. Kundi kubwa zaidi la mashabiki wa klabu hiyo maarufu kama ''Landscrona'' limesema kuwa klabu hiyo limelazimishwa kuwasajili wachezaji weus. Wamesema, wachezaji ambao wanashiriki katika mapenzi ya jinsia moja, ni aibu kwa mji wao ambo una heshima zake. Lakini mkurugenzi wa klabu hiyo wa masuala ya michezo, Dietmar Beiersdorfer,amesema wachezaji wa klabu hiyo husajiliwa bila kuzingatia mahala au nchi wanakotoka,rangi au dini wanayoshiriki. Hata hivyo klabu hiyo ya Zenit, imethibitisha kuwa inafahamu umuhimu wa uvumilivu. Hadi mwanzo wa mwaka huu, klabu ya Zenit ndiyo iliyokuwa klabu ya pekee inayoshiriki katika ligi kuu ambayo haikuwa na mchezaji mweusi. Mapema mwaka huu klabu hiyo Zenit walimsajili mshambulizi...

Hamman ajiuzulu kutoka FIFA

Image
Aliyekuwa makamu wa rais wa FIFA Mohamed Bin Hammam Mohamed Bin Hammam ametangaza ramsi kuwa amejiuzulu kutoka kwa nyadhifa zake katika kamati kuu ya shirikisho la mchezo wa soka duniani FIFA na pia kama rais wa shirikisho la mchezo wa soka barani Asia, AFC. Hamman, ameliambia shirika la habari AFP kupitia barua pepe, kuwa amejiuzulu kutoka nyadhifa hizo siku Kumi, baada ya kamati kuu ya maadili ya FIFA kuanzisha upya uchunguzi kuhusiana na madai ya ufisadi dhidi yake. FFIA imethibitisha kupokea barua kutoka kwa Hamman ya kujiuzulu, lakini imekariri kuwa kamati yake ya madili imesalia kuwa uhuru na ina uwezo kwa kuchukua maamuzi kuhusiana na masuala mbali mbali, licha ya wanaohusika kujiuzulu. Katika misingi hiyo, FIFA imesema ripoti yake ilionyesha kuwa Mohammed Bin Hamman, alikiuka kifungu cha 19 cha sheria zake wakati alipokuwa rais wa AFC na mwanachama wa kamati kuu ya FIFA, kati ya mwaka wa 2008 hadi mwaka wa 2012, hatua iliyopelekea kamati hiyo kumpiga marufuku ...