Wafanyakazi wa afya wawili zaidi wauawa

Raia wa Pakistan
Raia wa Pakistanwakiomboleza kifo cha wafanyakazi wa afya
Polisi nchini Pakistan wamesema kuwa watu waliojihami kwa bunduki wamewauwa watu wawili wanaohusika katika kampeni ya utoaji chanjo dhidi ya ugonjwa wa kupooza au polio, siku moja tu baada ya wafanyikazi watano wa afya kuuwawa kwa kupigwa risasi.
Msemaji wa shirika la umoja wa mataifa kuhusu watoto UNICEF, amesema kuwa sasa wamelazimika kuahirisha kampeni hiyo kote nchini Pakistan, kutokana na sababu za kiusalama.
Mashambulizi ya hivi punde katika mji wa Peshawar, yamepelekea mauaji ya mwanamke aliyekuwa akisimamia zoezi hilo la utoaji chanjo, dereva wake na mtu aliyekuwa akitoa chanjo.
Viongozi wa Taliban wanasema kampeni hiyo dhidi ya ugonjwa wa polio ni kisingizio cha kufanya ujasuisi dhidi yao.
Serikali ya Pakistan imesema haitakata tamaa katika juhudi za kutokomeza ugonjwa huo nchini humo na imeapa kukabiliana na wapiganaji hao wa Taleban kwa ushirikiano na jamii ya Kimataifa

Comments

Popular posts from this blog

FIELD REPORT ON BTCIT 2012

Afanya mapenzi na mifupa ya maiti